Nyumba SACCOS Ltd imeanzisha huduma mpya ya mkopo wa Ujenzi kwa wanachama wake, ambapo mwanachama ataweza kukopa pesa kwa manunuzi ya vifaa vya ujenzi. Riba itakuwa kiwango cha asilimia 1 kwa mwezi au asilimia 11 kwa mwaka kwa kutumia mfumo wa salio la mkopo linalopungua (Reducing Balance Method).
Kiwango cha kukopa ni hadi Shilingi Milioni hamsini (Tshs. 50,000,000/=), kiasi cha mkopo hakitazidi mara tatu [3] ya Akiba ya mkopaji. Ulipaji wa mkopo utakuwa kwa kipindi kisichozidi miezi sitini (60).