Mkopo huu hutolewa kwaajili ya Sikukuu na mwanachama atakopeshwa kiasi kisichozidi Laki tano (Tshs. 500,000/=) kwa riba ya 2.08%, marejesho ya mkopo huu yatakua kwa kipindi cha miezi 6.
Mwanachama hataruhusiwa kupata mkopo mwingine wa Sikukuu endapo hatokuwa amekamilisha marejesho ya Mkopo wa Sikukuu uliotangulia.
Mwanachama anaweza kukopa mkopo wa Sikukuu hata kama ana mkopo mwingine kama vile mkopo wa maendeleo, bila kuathiri vigezo na masharti (1/3 ya mshahara).
Muombaji atahitajika kujaza fomu ya maombi na kuiwasilisha ofisi za Chama.