info@nyumbasaccos.co.tz +255 746 436 049 

SERA YA UWEKEZAJI

Sera hii inatoa mwongozo wa kisheria na uwazi katika uwekezaji wa aina mbalimbali utakaofanywa na chama kwa kuzingatia Sheria ya Vyama vya Ushirika Na.6

Fahamu Zaidi

MWONGOZO WA MATUMIZI YA MFUKO WA TAHADHARI

Huu ni mfuko unaowahusisha wanachama wote wa NYUMBA SACCOS LTD ambao wanatimiza wajibu wao kwa kuchanga Akiba kumiliki Hisa na kukopa mikopo kutoka kwenye Chama.

Fahamu Zaidi

MASHARTI YA CHAMA

Masharti ya chama cha ushirika wa akiba na mikopo nyumba (Nyumba Savings and Credit Cooperative Society Ltd – NYUMBA SACCOS LTD)

Fahamu Zaidi

nyumba saccos

Nyumba SACCOS ilianza tarehe 18 mwezi Juni 1969 kwa usajili namba 1904. Chama kilianza na wanachama 103 kama waanzilishi kikiwa na lengo la kuboresha mahitaji ya kiuchumi kwa wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa kwa kuwawezesha kuweka na kukopa kwa riba ndogo ikilinganishwa na riba zinazotolewa na ma-benki.

DIRA

Kuwa SACCOS kiongozi inayotegemewa katika utoaji wa huduma bora za kifedha nchini.

DHAMIRA

Kuboresha hali ya kijamii na kiuchumi kwa wanachama wetu kwa kutoa huduma bora na nafuu.

Fanya Maamuzi Sasa

Anza safari yako ya mafanikio na Nyumba Saccos wekeza akiba yako na kopa kwa uhuru kwa ustawi wa baadaye.

utawala

Nyumba SACCOS inajivunia uwazi, uwajibikaji, na uadilifu katika uongozi wetu, ukilenga kuwahudumia wanachama wetu kwa
ufanisi na kufikia malengo ya maendeleo endelevu.

Grace Amini

Meneja

Ruth Charles

Mhasibu

Dennis Masinda

Afisa Tehama

Winfrida Kasonso

Afisa Mikopo

Veronica Mkumba

Mhudumu wa Ofisi

HABARI Na MATANGAZO

Pata habari za hivi karibuni kuhusu huduma zetu, fursa za uwekezaji, na taarifa muhimu kwa wanachama wetu,
kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi kwa ustawi wao wa kifedha.

Huduma za Mikopo na Uwakala wa Fedha

Habari Ndugu wanachama. Tunayo furaha kuwatangazia ya kuwa Huduma za Mikopo na Uwakala wa Fedha mtandao zimeanza kupatikana katika jengo la Kambarage House - Elevated Floor, karibu kabisa na ofisi za mauzo za Shirika la Nyumba la Taifa. Karibuni Sana

Akaunti za Benki

Habari Ndugu Mwanachama,Unakumbushwa kutoa taarifa mara tu unapofanya muamala kuja Nyumba SACCOS LTD kwa njia ya Benki au Uwakala wa fedha mtandao.”Pamoja Tujenge Uchumi”

ZIARA KWA CHAMA CHA WASIOONA TANZANIA (TLB) WILAYA YA TEMEKE.

CHAMA cha Wasioona Tanzania (TLB) Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam kimeishukuru Nyumba SACCOS Ltd kwa kuguswa na mahitaji yao, hivyo kuwawezesha kiasi cha fedha na fimbo za kutembelea. Pongezi hizo wamezitoa leo Juni 18, 2022 wakati uongozi wa Nyumba SACCOS Ltd ulipofanya ziara…